DIWANI ALIEUAWA AZIKWA JANA

 ALIYEWAHI kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Mwanza na
Diwani wa Kata ya Kisesa (CCM), Clement Mabina (56), amezikwa mchana huu
shambani kwake Kanyamati, Kisesa mkoani Mwanza. Mazishi hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, Waziri wa Nchi
Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wasira, viongozi wa
serikali, madhehebu ya dini, vyama vya siasa, wananchi na wakazi wa
Kisesa ambao wameungana na ndugu, jamaa na marafiki kumsindikiza
marehemu Mabina. Mazishi hayo yalitanguliwa na ibada iliyofanyika uwanja
wa Ngomeni-Kisesa, Mwanza








Socials