HAWA wa Nitarejea Afunguka "Wimbo wa Nitarejea wa DIAMOND Nauchukia Sana Umeniharibia Maisha Yangu



Unakumbuka Video ya Nitarejea ya Diamond? Basi yule msichana aliyeshirikiana naye katika huo wimbo hali yake si nzuri kisanii na kimaslahi pia kiasa cha kusema kuwa anauchukia huo wimbo kwani ndo umemuharibia Maisha
Hawa akihojiwa na Mlimani TV amefunguka na kusema kuwa Pamoja na Wimbo huo kuwa ndio uliomtoa Diamond Kimuziki lakini Diamond hakuwahi kumpa Hata Shiling 10 , Japo ameshawahi kumfuata na kumuomba msaada wakati tofauti tofauti lakini haikuwezekana kupata huo msaada ....Hawa amesema alitegemea nae angetoka lakini ameishia kuwa na maisha ya Dhiki huku mwenzake akitengeneza Hela za Maana ..


Alipoulizwa Kuhusu tuhuma za kutumia Madawa ya Kulevya baada ya kuona mambo hayaendi vizuri Hawa amesema hakuwahi kutumia Madawa ya Kulevya bali alijiingiza katika unywaji wa pombe sana baada ya Mwanaume aliyempa Mimba Kumkimbia hivyo alianza matumizi ya pombe kupunguza Mawazo ..


Hawa anasema Hamchukii Diamond ila Anapenda kumwambia akumbuke alipotoka na Arejee Nyumbani....

Socials