MDADA AFARIKI KWA KUANGUKA GHAFLA AKIWA NJIANI KUELEKEA KWA MGANGA WA KIENYEJI

Baadhi ya  vitu  alivyokuwa  navyo  Sharon:

Mwanamke  mmoja  aliyefahamika  kwa  jina  la  Sharon Justice Laiza, mkazi wa  Kilimahewa  jijini  Mwanza amefariki dunia  katika  mazingira  ya  kutatanisha   baada  ya  kudondoka  ghafla  akiwa  njiani  kueleakea  kwa  mganga  wake  aishiye  Kiseke, Ilemela  Mwanza... 

Kwa  mujibu  wa    mashuhuda  wa  tukio  hilo  lililotokea  juzi  saa  kumi  na  moja  jioni , mwanamke  huyo  alidondoka  umbali  wa  mita  kadhaa  kabla  ya  kufika  kwa  mganga  wake.

Baada  ya  kudondoka, mwanamke  huyo  alilazimika  kumpigia  simu  mganga  huyo  maarufu  kwa  jina  ustaadhi   akimtaarifu  kuwa  amedondoka   kabla  ya  kufika na  kwamba  anahitaji  msaada....

Taarifa  zinaarifu  kuwa, Mganga  huyo  alituma  vijana  wake  wakamchukue  kwa  kuwa  yeye  hakuwa  nyumbani  wakati  huo. Vijana  walifika  na  kumbeba, lakini  kutokana  na  hali   aliyokuwa  nayo  mwanamke  huyo, vijana  wale  walilazimika  kumpigia  simu  mganga  wakimtaka  aje  haraka  kwa  kuwa  hali  ya Sharon  haikuwa  nzuri....


Kitambulisho  cha kazi

Akisimulia  tukio  hilo, mganga  huyo  alidai  kuwa  baada  ya  yeye  kurudi  nyumbani, hali  ya  mwanamke  huyo  ilikuwa  ni  mbaya  zaidi  kiasi  cha  kushindwa  hata  kuleza  shida  iliyompeleka  kwake.

"Niliporudi  hakuweza  kunieleza  shida  yake  kutokana  na  hali  yake. Nilimuuliza   nikusaidiaje, akasema  nipeleke  Hospitali  ya  Mwananchi.

"Tulimpeleka  lakini   wakasema  wao  hawana  sehemu  ya  kumlaza  wakasema  twende  Bugando. Pale  Bugando  walisema  alikuwa  amebanwa  na  kifua  na  miguu  ilikuwa  imekufa  ganzi , hivyo  akalazwa.


"Wakati  huo  alikuwa  anaongea  kwa  shida. Aliniagiza  niende  kazini  kwake ( New  Mwanza  Hotel )  nikatoe  taarifa  na  kisha  nirudi  kesho  yake  asubuhi  maana  wakati  huo  ilikuwa  ni  usiku  wa  saa  nane.

"Kabla  sijaondoka, Daktari  alinambia  kuwa  mgonjwa  anataka  maji.Nikaenda  katika  duka  la  Bugando  kuangalia  lakini  wakati  narudi  nikakuta  ameshafariki  dunia....

"Baada  ya  tukio  hilo, nilirudi  na  kutoa  taarifa  kwa  balozi  na  kesho  yake  asubuhi  tukatoa  taarifa  kwa  serikali  ya  mtaa  na  polisi." Alisema  mganga  huyo

Akiongelea  kuhusu  uhusiano  wake  na  mwanamke  huyo, mganga  huyo  alidai  kuwa  amejuana  naye  alipomfuata  akiomba  msaada  wa  kupata  kazi.

"Tulifahamiana  naye  baada  ya  kuomba  nimsaidie  apate  kazi  baada  ya  kufukuzwa  alipokuwa  hapo  mwanzo. Nilifanya  mipango  yangu, akapata  kazi  New Mwanza  Hotel.  Sikuwahi  kumtibu  ugonjwa  wowote  mbali  na  msaada  wa  kupata  kazi"
Mganga  wa  jadi  (  kulia )  akiwa  na  vijana  waliombeba  mwanamke  huyo .

Wakiongea  na  mtandao  huu, afisa  mtendaji  wa  Kiseke, bi  Hellen Mcharo  na  mwenyekiti  wa  mtaa  wamethibitisha  kutokea  kwa  tukio  hilo  na  kwamba  mwili  huo  umehifadhiwa  hospitali  ya  Bugando  ukiwasubiri  ndugu  zake  toka  Arusha.

Socials