KUNDI LA WASANII KUJIUNGA CCM KWA PAMOJA...NI KUPENDA KWAO AMA KUNA USHAWISHI?

Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na Mtindo wa Wasanii wa Fani Mbali mbali kujiunga na Siasa hasa wasanii kutoka kambi ya Bongo Flava...Mfano Sugu , Vick Kamata, Afande Sele, Roma na Wengine...Hii imekuwa sasa kama staili ukichukulia kwamba wasanii hao wana ushawishi mkubwa kwa Jamii yetu ya Kitanzania
Jana kuna Kundi la wasanii ambao wamejiunga CCM...Nilipost habari hiyo na Watu wametoa hisia tofauti tofauti kuhusu tukio hilo la Wasanii Wengi kwa Pamoja kuingia CCM wengi wamekuwa na shaka kuhusu hilo na kuuliza maswali yasio na majibu ...Wasanii hao walionekana wakipanda ndege ya Fast Jet Kuelekea Mbeya kwa Makundi ...Je wewe Unaona ni sawa na wamejiunga kwa kupenda kwao ama kuna ka ushawishi ? 

Socials